Baada ya Taarifa iliyokuwa ikisambaa siku jana kuhusu mgomo wa wafanyabiashara jijini Dar es salam na mikoa mingine, Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Albert Chalamila ametoa tamko la kuwataka wafanyabiashara wote wa Mkoa wa Dar es salaam kujihepusha na mikumbo ya aina hiyo na kila mmoja kujitafakari
"maswala ya mgomo kwa wafanyabiashara yasichukuliwe kuwa ni jambo la pamoja kila mmoja awe na tafakari ya kutosha kabla hajafikia wazo hilo la kufunga biashara, mtu yeyote ambaye anaweza kuleta ubabe kutokusikilizana maana yake Serikali nayo inaweza kuamua kufanya hivyo hivyo jambo ambalo hiyo siyo falsafa hata kidogo ya Mhe Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania"
"Wote tuungane kuijenga dar es salaam migono sio suluhisho hata kidogo wala tusishabikie mwisho wa mgomo inaweza ikawa ni vita ndogo ambayo ikamhathiri ata asiyekuwa na hatia" Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam, Chalamila
Негізгі бет "MGOMO SIO SULUHISHO, MJITAFAKARI" RC CHALAMILA ATOA TAMKO KWA WAFANYABIASHARA WANAODAIWA KUGOMA
Пікірлер: 272