Aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Simiyu, Dk Yahaya Nawanda amepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Mkoa wa Mwanza na kusomewa shtaka moja la kulawiti katika kesi ya kulawiti.
Dk Nawanda amepandishwa kizimbani leo Jumanne Julai 9, 2024, mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama ya Mkoa wa Mwanza, Erick Marley na kusomewa shtaka hilo la jinai namba 1883/2024 na waendesha Mashtaka wa Serikali, Magreth Mwaseba na Martha Mtiti.
Kwa mujibu wa Mwaseba mshtakiwa (Nawanda) alitenda kosa hilo kinyume na kifungu namba 154 (1)(a) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu sura ya 16.
Mwaseba ameieleza mahakama kuwa mshtakiwa, Yahaya Nawanda anashtakiwa kwa kosa la kumwingilia kinyume na maumbile'kumlawiti' Tumsime Ngemela kosa analodaiwa kulitenda Juni 2, 2024 eneo la maegesho ya magari lililoko Rock City Mall wilayani Ilemela mkoani Mwanza.
Baada ya kumsomea Nawanda shtaka linalomkabili, Mwaseba ameieleza mahakama kuwa upelelezi wa shauri hilo umekamilika hivyo akaomba tarehe nyingine kwa ajili ya mshtakiwa kuanza kusomewa hoja za awali.
Hata hivyo, mshtakiwa, Dk Yahaya Nawanda anayewakilishwa na Wakili, Constantine Mutalemwa amekana kutenda kosa hilo kisha kuomba dhamana kwani kosa lake linadhaminika.
Baada ya maelezo ya pande zote, Hakimu Marley amesema dhamana kwa mshtakiwa iko wazi na kumtaka kuwa na wadhamini wawili, mmoja awe mtumishi wa Umma na mwingine wa sekta binafsi na bondi ya mali isiyohamishika yenye thamani isiyopungua Sh5 milioni.
Mshtakiwa ametimiza masharti ya dhamana na kuachiwa huku Hakimu, Marley akiahirisha shauri hilo hadi Julai 16, 2024, kwa ajili ya mshtakiwa kusomewa maelezo ya awali na kesi kuanza kusikilizwa.
MWISHO.
#samiasuluhuhassan #simbasc #yangasc #mashabiki #nbcpremeireleague #cafchampionsleague #cafconfiderationcup #ikulumawasiliano #entertainment #music #news #yangasc #simbasc #cafchampionsleague #mayele #highlights #cafconfiderationcup #riversunited #mashabiki #yangaleo #yanga #timuyawananchi #daimambelenyumamwiko #entertainment #music #news #magoliyasimba #magoliyayanga #magoliyote #magoliyamayele #mayele #aziziki #manara #manaraleo #ikulumawasiliano #magufuli #kikwete #mayele #singidabigstars #magoliyamayele #magoliyasimba #magoliyayanga #highlights #azamsportsfederationcup #chama #Shot #mamelodisundowns #alahlytv #alahlysc #miraj
Негізгі бет Mwanzo mwisho Nawanda alivyopandishwa Kizimbani, Mahakama yaamua haya
Пікірлер: 19