Katika mfululizo mpya wa makala kuhusu vijana walio chini ya miaka 30 tunaangazia vijana waliofanya vizuri na wanaoendelea kufanya vizuri katika teknolojia, siasa na kijamii kwa nchi za Afrika Mashariki na leo tunae Bi Zainab Abdallah ambaye ni Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo.
Akiwa na umri wa miaka 23 ndipo aliaminiwa kufanya kazi kubwa ya kumuwakilisha rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kama Mkuu wa Wilaya.
Licha ya hilo hakusita kukumbatia kipaji alicho nacho cha utunzi na ughani wa mashairi ambacho kimempa umaarufu mkubwa hasa siku za hivi karibuni.
#bbcswahili #tanzania #wanwake #talanta #uongozi
Негізгі бет 'Niliteuliwa nikiwa mwaka wa pili chuoni sitasahau maishani'
Пікірлер: 173