Othman maalim ni shekhe ambae anafaham nini atumie ktk elimu yake ni mtu ambaye lazima umuelewe yupo vizuri sana..... sasa ww unaepiga kelele halafu hujasoma dini shauri yako
@jumamnyage5395
4 жыл бұрын
Inaonekana kuna watu hata wasomi hawawajui uliza wasomi wa nchi hii akina nani ?
@farwatskitchen13
5 жыл бұрын
Ina thamani elimu. Vijana tusomeni kisawa Sawa elimu haswa elimu ya dini. Allah atujaalie hima na hamu ya kuitafuta elimu.
@hassankhamis7977
8 жыл бұрын
Nilickiza mawaidha mengi Sana ya huyu sheikh na hakuna hata mawaidha moja niliyomsikia akitukana watu wala kukejeli masheikh wenzake Mashaallah huyu sheikh ni msomii Sanaa...... Mungu amzidishie
@HababahappynewyearNuru
7 жыл бұрын
Hassan Khamis Kweli Maa Sha Allah ni Sheikh Mwenye HIKMA NA MWENYEZMUNGU AMJAALIE QABULI KWA KAZI ZAKE ZA KUELIMISHA UMMA...AMPE TAUFIQ...YY NA SOTE..AMIIIIN.
@khalfankhamis9083
5 жыл бұрын
Huyo kwa Tanzania mzima utamshindanisha nanan huyo hakuna shekhe ata mmoja anae muweza kwalolote mungu kanampa elimu na mungu amzidishie
@meena-ol6fo
4 жыл бұрын
Kati ya mashekhe wenye hekma na busara sijapataona
@bobsule4036
4 жыл бұрын
Masha Allah Shukran sheikh uko vizur sana Allah akuhifadh n akupe umri amiin
@engamidulutta1496
5 жыл бұрын
Sherkh uko sahihi na Allah akujalie wewe na sie ila wewe n mbora katika masimulizi ya hadithi vip unaonaje kama utaitafuta istoria ya maulid mwanzo wake kisha tunaokusikiliza tuamue inshaallah
@bashirkijoji3437
5 жыл бұрын
Ombi langu kwa waislamu Tusome tusikaririshwe kwenye DVD na tukawa masheikh,
@suleimanhemed9234
4 жыл бұрын
Mashallah shekh ujumbe ushafia waache wenye kupiga kelele wapige ila umefahamika sana Allah akuzidishie inshallah
@jumamnyage5395
4 жыл бұрын
Waislaam tunaipima kheri kupitia matendo ya mtume na maswahaba wake watukufu sio othmani maalim wala mwingine mavi yatabaki kua mavi ht ukiyapulizia pafyuum.
@ashaali4881
9 жыл бұрын
tunamsifu mtume sana kwa sababu mwenyeenzi mungu ame mtjma kwetu atufikishie dini ya uisilamu ambai indie dini ya haki na allhamdulilahi .Mtume [s.a.s]na maswahaba wake [r,a] wamefanya juhudi kubwa sana kutufikishia dini ya uisilamu.
@Mrmanguguru
13 жыл бұрын
Mashallah Sheikh Othman washushie vitu hadi wafahamu wenye kutaka kufahamu na wasio taka kufahamu basi waachie wenyewe.
@jumannejums9020
7 жыл бұрын
kila lakheri shekh wetu
@aliabdulla2447
6 жыл бұрын
MASHAALLAH SHEIKH OTHMAN MAALIM.
@rashidibrahim6763
7 жыл бұрын
mashallah mungu akujaze kwa faida juu ya maulidi shukran sana kwa ufafanuzi wako kuhusu maulidi
@hasanisaidishabani3879
2 жыл бұрын
Shekhe km mtu alikusikiliza ajue ukweli ubainifu si kwa kutafuta kasoro na mabishano umeeleza vzr sana allah akupe umri mrefu mnooo tena mnoooo wee nakupenda shekh kwaajili ya allah
@salamakhamis7245
5 жыл бұрын
Baaraka LLAHU fiiqu yaa Sheykh tumekuelewa. watu wa shekh googol hawatokuelewa milele. kazi yao fitna na farqa tu ktk ulimwengu huu
@jumamnyage5395
4 жыл бұрын
Anasema ibn kathiir Amma ahli sunna wanasema kwenye kila kitendo na neno lisilothibiti kwa swahaba hilo ni bidaa.
@birdofpry3897
6 жыл бұрын
Shukran sana sheikh wetu kwa kutuelimisha kwa undani zaid tunafaidika sana kwa uwepo wako Allah akupe elmu zaid uzidi kutuelimisha
@sangokipozi4611
2 жыл бұрын
Allahumma Aamiin ya Rab. Allah sub han wa taala akupe umri mrefu na afya njema ndugu yetu. Allah akujaalie pepo/ Jannatil firdaus miongoni mwa waja wake wema in shaa Allah. Aamiin ya Rabbal Alamiin
@hassankhamis7977
8 жыл бұрын
Mashaallah... Huyu sheikh si kidogo.. Mungu amzidishie... Mti
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
kwamba Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amefanya hiyana katika kufikisha ujumbe (aliopatiwa na Allaah), kwani Allaah Anasema: “Leo Nimewakamilishieni Dini yenu, na Nimetimizieni neema Yangu na kuwaridhia Uislamu kuwa ndio Dini yenu”(5:3). Hivyo jambo ambalo halikuwa Dini siku hiyo halitakuwa leo ni katika Dini” (Al-I‘tiswaam ya ash-Shaatibiy, Mj. 1, uk. 49). Ya Sita: Yeyote mwenye kufanya amali hii anakwenda kinyume na sheria na kujitia katika mashaka kwani sheria ishaweka yale yanayotakiwa kufanywa na mja kwa njia na namna maalumu. Na viumbe wamefupishiwa juu yao kwa kuwekewa amri na makatazo na ikatujulisha kuwa yaliyo kheri yapo ndani yake na shari ni kuyaepuka, kwani Allaah Anajua yaliyo na maslahi kwa waja. Na Allaah Hakutuma Mitume na wala Hakuteremsha Vitabu isipokuwa aabudiwe Yeye kwa yale Anayotaka Yeye. Hivyo, yule mwenye kuzua Bid‘ah hii (yaani ya Mawlid) ameyatupilia mbali haya yote akidai kuwa ipo njia nyingine ya kufanya 'Ibaadah na kwamba yale mambo yaliyoletwa na sheria si lazima. Hivi ni kama kusema kwa ulimi wa hali hii yake kuwa mtungaji sheria anaelewa na yeye pia anajua. Na huenda ikawa kuwa yeye anafahamu jambo ambalo mtungaji sheria halijui. Ametakasika Allaah, huu ni uongo mkubwa wa wazi kabisa na uhalifu wa hatari na dhambi ya wazi na upotevu mkubwa. Ya Saba: Hakika katika kusimamisha bid‘ah hii ni kupotosha msingi miongoni mwa misingi ya sheria, nako ni kumpenda Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa
@mozeymbuna4960
3 жыл бұрын
🙏
@sadasada1291
6 жыл бұрын
SHEKHE OTHUMAN MAALIM ALLAAH AKUZIDISHIE KHER NYUNG NA BARAKA NAKUPENDA KWA AJILI Y ALLAH
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
uoni, ikhlasi na kuwa na nia ya kutaka kuifikia haki na kila mtu ayasome kwa ajili ya kupata mazingatio na bila ya kufuata wanavyuoni wa nchi zao au wengineo kimbumbumbu au madhehebu yao au ada na mazoea yao. Ikiwa yaliyo ndani ni haki tuyakubali kwa moyo mkunjufu na hivyo kwayo tuende katika kumtii Allaah na Mtume Wake, ambao wametuamrisha kufuata haki na ikiwa kuna batili ndani yake au makosa, tunakushuhudisha kwa Allaah usiwe ni mwenye kufuata hayo kwani sisi hatufai kufuata isipokuwa yale ya haki ambayo yana dalili katika shari‘ah yetu tukufu. Tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Atuwafikishe sote katika kufuata njia nyoofu ambayo ametuchagulia Mtume wetu na Allaah Ndiye Mwenye kutia tawfiki na Kwake ndio mategemeo yetu. 2.0 HISTORIA Yeyote mwenye kutazama maisha ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na historia ya Maswahaba zake (Radhwiya Allaahu ‘anhum), Taabi‘iyna na waliowafuata kwa wema mpaka kufikia zaidi ya mwaka wa 350 Hijri hatumuoni hata mwanachuoni mmoja wala mahakimu (viongozi) na wala watu wa kawaida waliokuwa wakifanya mawlid au wakaamrisha au wakahimiza au wakazungumza juu yake. Amesema al-Haafidh as-Sakhawiy: “Shughuli za kufanya Mawlid matukufu hayakupokelewa na watangu wema (Salafus Swaalih) wa karne tatu bora za mwanzo. Kwa hakika jambo hili lilizuliwa baada yake” (Imenukuliwa kutoka kwa Subulul Hudaa war Rashaad cha As- Salihiy, Mj. 1, uk. 439).
@zulfaalnabhanzulfaalnabhan8653
8 жыл бұрын
mashaa ALLAH darsa mzuri ALLAH akupe umri mrefu uzidi kutupatia mengi mazuri (shukran wa jazakaLLAH kheyr)
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
Faatwimiyyuun ‘Ubaydiyyah: “Wao walijidhihirisha kwa watu kuwa wao ni masharifu (watukufu) kutoka kwa Faatwimah hivyo wakamiliki na kutawala ardhi na kuwatendesha nguvu waja. Na wametaja kipote cha Wanachuoni wakubwa kuwa wao hawakustahiki hilo na nasaba yao si sahihi bali walikuwa wanajulikana zaidi kwa banu ‘Ubayd. Na baba wa ‘Ubayd alikuwa ni katika kizazi cha wakanaji Mungu na Mmajusi na inasemekana kuwa babake alikuwa Myahudi mfua vyuma kutoka Shaam. Jina la huyu ‘Ubayd lilikuwa ni Sa‘iyd, lakini alipofika Morocco alijiita ‘Ubaydullah na akajidai kuwa yeye ni katika ukoo wa ‘Alawi Faatwimiy na madai yake ya nasaba hiyo siyo sahihi. Yeye hakutajwa na yeyote miongoni mwa wajuzi wa nasaba za ‘Alawi, kipote kikubwa cha wanavyuoni wametaja kinyume cha hayo. Alijinasibisha na Bani Mahdiyyah wa Morocco, naye alikuwa Zindiyq muovu, adui wa Uislamu na alijidhihirisha Ushia wake. Alikuwa na hima ya kuiondoa mila ya Kiislamu pamoja na kuwaua mafaqihi wengi pamoja na wanavyuoni wa Hadiyth. Kusudio lake kubwa lilikuwa kuwaondosha kabisa ili dunia ibaki na wanyama pekee na hivyo kumakinika katika kuleta uharibifu katika itikadi zao na kuwapoteza lakini Allaah
sheikh you are top just continue to teach them especially who called as SALAFYYYYYY
@fatmahussein6085
2 жыл бұрын
sure these people calling themselves salafy we suppose to teach them
@anonymousahmadi3826
7 жыл бұрын
Maashaallah wallahi sheikh uthman anafaa awe muislamu muahmadiyya. I love you sheikh for the sake of Allah. The promised messiah and imam mahdi sayyidina mirza ghulam ahmad as has already come to save the Muslims as the hakam and adl. Please accept him and be saved. Amin.
@yasintabenedict3561
2 жыл бұрын
Alhamdulillah shekh allah akuzidishie elimu na uelewa mkubwa amin
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
“Leo Nimekukamilishieni Dini yenu, na kukutimizieni neema Yangu, na Nimekupendeleeni Uislamu uwe Dini yenu”(5:3). Na yule anayesema kuwa Mawlid ni 'Ibaadah nasi tunamuabudu Allaah kwayo anaikadhibisha aayah hii, na kufanya hivyo ni kumkufuru Allaah Aliyetukuka. Na akiwa anaiswadiki aayah hiyo atalazimika kusema kuwa Mawlid si 'Ibaadah. Kukubali kuwa ni 'Ibaadah ni kama unampatiliza Allaah na Mtume Wake kwamba hawakutuonyesha 'Ibaadah hii tukufu ambayo tunajileta kwayo karibu na Allaah na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Na akisema kuwa mimi sisemi kuwa jambo hilo ni 'Ibaadah wala kuwapatiliza Allaah na Mtume Wake, naye anaamini aayah hii, atalazimika kurudi katika kauli ya haki ya kwamba jambo hili ni uzushi ulioingizwa katika Dini. Tunamuomba Allaah Atuongoze na Waislamu wate kwa Analolipenda na la Kumridhisha. Ya Tano: Kufanya na kujihimiza katika uzushi huu wa Mawlid ni kama mtu anamtuhumu Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa alifanya hiyana na hakuwa ni mwenye kutimiza amana, tunajilinda kwa Allaah kwa hilo. Hii ina maana ya kuwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alificha kwa Ummah huu na hakuwaonyesha 'Ibaadah hii tukufu ambayo inamkaribisha mwenye kuifanya na Allaah. Amesema Imaam Maalik (Radhwiya Allaahu ‘anhu): “Yeyote mwenye kuzua katika Uislamu Bid‘ah ambayo anaiona ni njema, bila shaka amedai ya
@hamzaswaibu9470
4 жыл бұрын
Haujaeleweka shekh toa aya inayokataza maulidi mbona shekh othumani ametoa vitu vinaeleweka Sanaa ...lakini kama hutaki maulidi tumuwachie Allah ndiye atakae tuhukumu kama nimetumia kauli ikakuhudhi nisamehe hakuna mkamilifu
@hasanisaidishabani3879
2 жыл бұрын
Shekh ameongea kiswahili sana kukuelimisheni sana kwani ibada sikila jambo analolizia allah shekh sasa utakiwi kuangalia nnje jina angalia yanayofanyika nenda kwenye mauridi siku moja kaa fany uchunguzi wallah utaona ukienda weka uchunguzi utaona mm nimeona mauridi ibada kubwa tena sana wallah mm nasoma mpk sasa nimetafuta chuo huu mwaka wa7 sababu maurid nilitoka sikumoja nikaenda maulidini sitosaau alisimama shekh waridi kutoa mawaidha bas yaliniingia nayale niliyoyaona pale wallah nasema mtu akiikosoa mauridi namuona ayuko sawa
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
Na Mawlid hayawezi kufana bila beti za burdai, Allaah Atuongoze na Atusaidie. Na lau kama hakungekuwa na uharibifu mwengine isipokuwa huu basi ingetosha kuharamisha na kutoa onyo kali kuhusu jambo hilo. Ya Kumi na Tatu: Kufurahi siku hii na kulisha watu na kutoa sadaka ndani yake na kudhihirisha bashasha kwa yale mapenzi kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Na wameafikiana wanachuoni wote kuwa siku hii ya tarehe 12 Rabi‘ul Awwal ni siku aliyefariki Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Vipi sasa watu watakuwa wanafurahi kwa siku kama hiyo? Anas bin Maalik (Radhwiya Allaahu ‘anhu) anatuhadithia kuwa hakuna siku ambao watu wa Madiynah walikuwa na furaha ya hali ya juu kama siku aliyohamia Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) katika mji huo. Na hakuna siku ya huzuni kabisa kwa watu wa Madiynah kama siku aliyoaga dunia Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Inaonekana kama sisi tunakwenda kinyume na maadili ya wale watu bora waliokuwa wakimpenda Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) hata kuliko nafsi zao wenyewe. Ama siku aliyozaliwa wanavyuoni wametofautiana sana kama tulivyotangulia kueleza hapo awali. Hivi itakuwaje 'Ibaadah kubwa yenye kumleta karibu mja na Allaah iwe katika siku ambayo watu wametofautiana. Ibn Hajar amesema katika kuisherehesha Hadiyth Na. 3641 kwamba wametofautiana wanavyuoni katika mwaka hasa aliozaliwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi
@amalakh1990
12 жыл бұрын
allhhu akbar .. mungu atoungoze ktk njia ya kheri. haifai kwa kila sheikh kujiona yeye ndo yuko juu zaidi kuliko mwengine ,than huwezi kuharamisha kitu cha kheri . bali cha kheri kikichanganyika na shari ndipo kinnatenganishwa na sio kuachwa wala kusema ni bidaa
@adamufadhili8056
7 жыл бұрын
allah akubaarik sh.othman maalim.mana napenda sana darsa zako.
@sayyidalishariff6068
3 жыл бұрын
Mashallah. Good education. Allah yahfadh hum.
@mussakimweri2979
Жыл бұрын
Maashaallah tutufuteni ilim waisilamu maana tusiokuwa na ilim tunabaki njia panda nifate wapi
@twahahango3968
3 жыл бұрын
Wallah Allah akulipe jannat fordaus
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
viumbe vyake”. Na kwa wengine: “Huyu ni Mtume wa Allaah na dalili ya Allaah”. Na kwa wengine: “Yeye ni Allaah, Muumbaji, Mwenye kuruzuku”. Hapana Mola muabudiwa wa haki ila Allaah tu, Naye Hana mshirika, Ametukuka na Hana upungufu wala kasoro aina yoyote kwa yale wanayoyasema madhalimu kwa kiburi kikuu. Alipoangamia alichukua hatamu za uongozi mtoto wake anayeitwa, Qa’im, naye alizidisha shari yake juu ya uovu wa babake maradufu. Akatoka na kuwatusi Manabii na alikuwa akinadi masokoni na sehemu nyenginezo: “Mlaanini ‘Aishah na mumewe. Mlaanini pango na vinavyounganishwa”. Ee Allaah! Mswalie Nabii Wako na Maswahaba zake na wakeze walio twahara na uwalaani hawa makafiri walioasi na kuvuka mipaka katika ukanaji wa Allaah na Uwarehemu waliopambana nao na ikawa ndio sababu ya kuing’oa mizizi na utawala wao. Waislamu katika zama za utawala wao walipata dhiki na shida kubwa kwa ukatili, kiburi na ujeuri wao uliochupa mipaka. Na juu ya Mawlid ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kama tulivyoona asli yake na mwanzilishi wake ni kutokamana na Baatwiniyyuun (Faatwimiyyuun) waliokuwa na asli ya Kimajusi Kiyahudi waliohuisha mwito wa watu wa msalaba. Na hapa tunawaambia ya kwamba: Je, inajuzu na kusihi kuifanya chimbuko letu katika 'Ibaadah ni kutoka kwa watu hawa? Nasi tunarudia mara nyingine tena kuwa zile karne zilizo bora na kufadhilishwa ambazo waliishi watangu wetu wema hakukuwa na athari wala kufanywa mfano wa hizi 'Ibaadah. Hawakufanya wao wala wale waliokuwa na
@abdulkarim7856
7 жыл бұрын
جزاك الله خيرا
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
Watu wa kwanza kuzua kile kinachoitwa Mawlid ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ni Bani ‘Ubayd ambao walikuwa wakijulikana kama Faatwimiyyuun. Haya yametajwa na Wanachuoni wengi mfano Mufti wa Misri wa zamani, Shaykh Muhammad Bakhiit al-Mutii‘y katika kitabu chake Ahsanul Kalaam Fi maa Yata‘alaq Bis Sunnah wal Bid‘ah Minal Ahkaam; Shaykh ‘Ali Mahfuudh katika kitabu chake Al-Ibda‘ Fii Madh- har al-Ibtidaa‘; Shaykh Isma‘iyl al-Answaariy katika kitabu chake Al-Qawlul Fasl Fiy Hukmil Ihtifaal Bi Mawlid Khayrir Rasuul. “Wa mwanzo walioyazua Mawlid huko Cairo ni watawala wa Kifaatwimiyyah (Mashia) katika karne ya nne. Walizua Mawlid aina sita: Mawlid ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), Mawlid ya ‘Aliy (Radhwiya Allaahu ‘anhu), Mawlid ya Bibi Faatwimah (Radhwiya Allaahu ‘anha), Mawlid ya Hasan (Radhwiya Allaahu ‘anhu), Mawlid ya Husayn (Radhwiya Allaahu ‘anhu) na Mawlid ya Khalifa aliyekuwepo” (‘Ali Mahfuudh katika kitabu chake al-Ibda‘ Fii Madh-har al-Ibtidaa‘, uk. 251). Je, Wanachuoni wamesema nini kuhusu hii Dola ya Faatwimiyyuun ‘Ubaydiyyah ambayo imeanzisha jambo hili (Mawlid ya Mtume)? Amesema Imaam Shaamah, mwana-historia na Muhaddith (aliyeboboea katika mas-ala ya Hadithi za Mtume [Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam]), mwandishi wa kitabu ar-Rawdhatayn Fiy Akhbaar Dawlatayn, uk. 200 - 202 kuhusu
@abuahmad1206
5 жыл бұрын
Ajab shekh wasema maulid ina faida Allah akuongoze
Funga mdomo wewe we ndio mnaoambiwa mkasome huwezi kumfikia huyu ahekhe nyie ndio mnaougawa uislamu
@ahmadsalim4417
4 жыл бұрын
Wewe ninani unaemuonea shekhe ajabu ikiwa hata alifu huna???? Jitathmini kijana kaachini usome achana na mashekh Google
@abuahmad1206
4 жыл бұрын
Maulidi yatoka wapi kuna pahal mtume wetu katufunza
@abuahmad1206
4 жыл бұрын
@@suleimanhemed9234 mtume wapi katufunza nipe hadith moja ama Aya tumeambiwa tumswalie si kumfanyia birthday
@engamidulutta1496
5 жыл бұрын
Alafu mashekh mmesoma kwann kila mtu analindima kwenye mimbali yake kwa nn msikutane mkatafuta suruu kwel Allah atatunusur kwa utengano huu
@bayouhd6729
5 жыл бұрын
MaashaAllah
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
Inatutosha Hadiyth hii tukufu: Imepokewa kwa Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu), amesema: Alikuja mtu kwa Mtukufu wa Daraja (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na akasema: “Yaa Khayral Bariyyah (Ewe mbora wa viumbe)”. Akasema Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Huyo ni Ibraahim ('Alayhi salaam)”. (Muslim). Allaah Anasema: “Alimchukua Ibraahiym kuwa kipenzi chake”. Haya yanafanywa leo katika Mawlid, ambamo kunatumiwa mali mengi na kuimbwa ndani yake nyimbo zinazomtukuza Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwa aina kubwa na kuvuka mipaka katika hilo. Na katika beti nyengine ni kumpatia hasa sifa za ubwana ambazo Anastahiki Allaah peke Yake. Ya Kumi na Moja: Bid‘ah ya Mawlid ni kuwa tumevuka mipaka yanayokubaliwa na sheria na tumevuka mipaka katika tuliyoamriwa katika kumpenda Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na tumevuka mipaka katika kusimamisha siku kuu za Kiislamu. Hakika ni kuwa hakuna katika sheria yetu isipokuwa 'Iyd mbili na atakayezua ya tatu basi atakua amevuka mipaka ya kisheria. Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) anaeleza ya kwamba alipohama Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) Madiynah walikuwa na siku mbili
@alhaddajmohammed4768
3 жыл бұрын
Miongini mwa dalili/ishara as Kiama (mwisho wa dunia) ni kukatana mapande kwa Wasomi/Maulamaa. Masheikh wetu wa Zama hizi wamezidi kupigana mapande na ni mtihan kwa Maamuma. Inshaallah Allah atujalie tuhtalafiane lakini tusifarakane ili inshaallah tuupate mwisho mwema.
@alirashid4291
11 жыл бұрын
nikweli uyu ndo mwalim wa waalim
@abuubakarhassan8021
6 жыл бұрын
Allah Akbar ni kweli shehk wangu
@sarahsalim1175
12 жыл бұрын
mashaallah .
@jumamnyage5395
4 жыл бұрын
Hakuna kheri isiyofanywa na mtume na maswahaba . Akuna kheri ya kubuni kheri imeshafanyika tangu zama izo huuu wa Leo ni uzushi mtupu ht mkiupamba vp
@user-qe8xp6ii1u
3 жыл бұрын
Huyu Akili hana kabisaaa,Mzushi na ni Muongo.Hana Elimu hakika.Na hawez isema Hadith hiyo Mzushi kama wew Athuman.
@safinabakari9140
7 жыл бұрын
SHAIKH OTHMAN MAALIM, Huwa hapendi kuongea mada zenye kugawa watu, isipokuwa watu walimtukana sana kwa kumwita shaikh wa bidaa sijui shaikh wa maulid na kuanza kumdharau ndio akawapasha. usidhani wanasherehekea maulid ni watu mazuzu.......Eti niulizeni suali lolote mlilokuwa nalo.....vijana wamesoma miaka mitatu madina basi fujo lingi.
@rajabfaki6159
5 жыл бұрын
mashaallah Shekh othmani mungu amzaidishie
@kassimomar5542
5 жыл бұрын
Safina Bakari ok
@swabirali1276
3 жыл бұрын
Nakupenda kwa Ajili ya Allah
@yahayaramadhani
Жыл бұрын
Shekhe Allah akulipe kher
@jeranibanzi2127
4 жыл бұрын
Ahsante Kwa kutujuza
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
“Na tahadharini na mambo ya kuzuliwa kwani kila uzushi ni upotofu” (Abu Daawuud, at-Tirmidhiy, Ahmad, Ibn Maajah na ad-Darimi kutoka kwa Abi Najiih al-‘Irbaadh bin Saariyah [Radhwiya Allaahu 'anhu]. At-Tirmidhiy amesema hii ni Hadiyth Hasan Sahiyh. Isnadi yake ni Sahihi na imesahihishwa na Ibn Hibbaan). Na katika riwaya nyingine: “Na kila upotevu ni wa motoni”. Na kauli yake: “Kila uzushi ni upotofu” ni sentensi ya kijumla na inaingia kila jambo lililozuliwa ambalo halina asili na msingi katika Dini ya Allaah. Na wanavyuoni wameafikiana kwa hilo, hivyo ni uzushi mpotofu unaompeleka mwenye kufanya kuingia Motoni, Allaah Atuepushe sote na adhabu hiyo ya moto. Ya Tatu: Yeyote mwenye kufanya bid‘ah hii hatapata ujira kwa kitendo hicho bali atarudishiwa mwenyewe kwa kauli ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Mwenye kufanya amali isiyokuwa na hukumu yetu, itakataliwa” (Muslim kutoka kwa ‘Aaishah [Radhwiya Allaahu 'anha]). Na katika jambo hilo haitoshi kuwa mtu ana niya nzuri bali hapana budi kumfuata Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Ya Nne: Allaah Aliyetukuka Anasema:
@masouddaud4075
3 жыл бұрын
Nimekaa kusikiliza maiwadha haya. Sijaona poit ya uhakika bado. Jamani tusomeni huu sio kweli kabsa
@swabirali1276
3 жыл бұрын
Hujaona point gani na KZitem yenyewe haikuwa wakati wa mtume lakini ni vizuri kuitumia kwa wema
@imranbanda3963
Жыл бұрын
Masha Allah
@yanifaakukufaa9032
12 жыл бұрын
maneno yamewaingia lkn ukweli sh yupo juu na elimu yake ipo kichwani ni watu wachache km hao
@ahmadsalim4417
4 жыл бұрын
Wale vilaza sioni ata mmoja akichomoa pua yake hapa hahahahaaa
@isamkwizu3342
7 жыл бұрын
umefanya moyo wangu kujua jahannam ni mbaya
@abdallahhemedi8028
5 жыл бұрын
anapiga story mtume na maswahaba walifanya hayo mangoma ya maulidi ahaaaa wanaogopa wanajua hawatopiga mpunga teteeni kula pilau
@swabirali1276
3 жыл бұрын
@@abdallahhemedi8028 wakati mtume anaingia madina tari lilipigwa na haikukatazwa
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
Sunnah zake na kujitolea mhanga kwa mali yao, familia zao na hata nafsi zao. Allaah Awaridhie kwa yale waliyokadimisha ili kuundeleza Uislamu. ni jambo ambalo lajulikana kuwa Allaah Amewaridhia na Kuwataja katika aayah kadhaa za Qur-aan na pia Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amewaridhia kwa waliyotanguliza. Na yeyote mwenye kuwatuhumu basi yeye mwenyewe ima atakuwa ni kafiri wa dhahiri au mnafiki. Allaah Anasema: “Kwa hakika Allaah Amewapa radhi Waumini walipofungamana nawe chini ya mti; na Alijua yaliyomo nyoyoni mwao, na Akawapa kushinda kwa zama za karibu” (48:18). Na Amesema tena Aliyetukuka: “Na wale waliotangulia wakawa wa kwanza katika Uislamu - Muhajiri na Ansari, na wale waliowafuata kwa mwendo mzuri-Allaah Atawapa radhi, nao wamridhie na Amewaandalia mabustani yapitayo mito mbele yake, wakakae humo milele. Huku ndiko kufuzu kukubwa” (9: 100). Imepokewa kwa Anas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Dalili ya Imani ni kuwapenda Answari na dalili ya unafiki ni kuwachukia Answari” (Al-Bukhaariy na Muslim). Imepokewa kwa al-Baraa’ bin ‘Aazib (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Hawapendi Answari isipokuwa Muumini na hawachukii Answari
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
Na hii imejumlisha ghuluw aina zote katika Itikadi na amali za 'Ibaadah. Na inajulikana kabisa kuwa sababu ya shirki ambayo imepatikana kwa wanadamu ni kuvuka mipaka ya sheria katika kuwatukuza watu wema. Imepokewa na Al Bukhaariy kutoka kwa Ibn ‘Abbaas (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba: Allaah Aliyetukuka amesema: (Na wakasema: Msiwaache miungu yenu, wala msimwache Wadda wala Suwaa' wala Yaghutha, wala Yau'qa, wala Nasra.). Akasema haya yalikuwa majina ya watu wema katika kaumu ya Nuuh. Watu hawa walipoaga dunia, shetani alikuja kwa kaumu yao na kuwashawishi wajenge jengo la ukumbusho katika sehemu walizokuwa wakikaa na waweke ndani yake sanamu na waziite kwa majina yao. Walifanya hivyo, nao hawakuabudiwa mpaka walipoaga dunia na elimu ikasahauliwa”. Na fananisha yale yaliyotokea kwa kaumu ya Nuuh ('Alayhis salaam) mbali na kuwa hawakuwa ni wenye kuabudu chochote hapo mwanzo lakini baadae wakaingia katika shirki. Na sababu ya haya, nayo ni njia moja ya ghuluwna utazame yanayotokea katika Mawlid kwa kupatikana shirki kwa kumuomba asiyekuwa Allaah na kumpatia Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) sifa za uungu kama kupelekesha kwake mambo katika huu ulimwengu na kujua kwake elimu ya ghaibu.
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
Huu ni mwito kwa kila Muislamu anayetaka kufikia kwenye haki na awe ni mwenye kumuabudu Allaah kwa uoni na elimu ya wazi kabisa. Ndugu Waislamu! Kwa yakini kila mmoja wetu ana mapenzi makuu katika vifua vyetu kwa Mtume wetu mtukufu na kipenzi na ruwaza njema na Imamu wetu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), pamoja na familia yake na Maswahaba zake na wenye kuzifanyia kazi Sunnah zake na kufuata uongofu wake mpaka Siku ya Qiyaamah. Mahaba haya ni msingi mkuu wa Dini yetu na yeyote asiyempenda Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) anakuwa kafiri na tunajiweka mbali sana na Allaah kwa kumchukia na kumbughudhi, na hiyo ni sifa ya wanafiki. Allaah Anatuelezea kuhusu wao: “Bila shaka wanafiki watakuwa katika tabaka ya chini kabisa katika Moto. Hutamkuta kwa ajili yao msaidizi (yeyote)” (4:145). Tunawekea makala haya mafupi kwa unyenyekevu baina ya mikono na macho yenu ili muyasome kwa
@fadhilimakore6142
5 жыл бұрын
Allah atunufaishe kwa elimu yako
@didahkassim5844
10 жыл бұрын
Mashallah nakukubali uko deep
@adinanisaidi777
3 жыл бұрын
Allah akujaalie heri sheikh wangu
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
Na miongoni mwa uovu wao ni kuwa walikuwa wakiwaamrisha makhatibu kwa hilo (yaani wao ni Alawiyyah Faatwimiyyuun) na hayo yalikuwa yakisemwa juu ya minbar na wakiandika katika kuta za Misikiti na sehemu nyinginezo. Na alihutubu yeye mwenyewe mtumishi wao kwa jina Jawhar, aliyeteka nchi ya Misri na kujenga mji wa Cairo. Alisema ndani yake: “Ewe Mola mswalie mja wako na rafiki yako tunda la Unabii na dhuria wako mwenye kuongoza muongofu anayepelekesha mambo. Naye ni Abi Tamiym Imam Mu‘iz-ud-Diinil Llah, Amiri wa Waumini kama ulivyowaswalia baba zake walio tohara na waliomtangulia kwa kuchaguliwa, maimamu waongofu”. Amesema uongo adui wa Allaah, hakuna kheri kwake wala kwa watangu wake wote wala kwa dhuria wake waliobakia na kizazi cha Unabii tohara miongoni mwao. Na yule mwenye lakabu ya Mahdi, laana ya Allaah iwe juu yake aliwachukuwa wajinga na kuwasalitisha kwao wale wenye fadhila. Alikuwa akiwatuma kwenda kuwachinja mafakihi na wanavyuoni katika firasha zao. Na akawasaliti Waislamu kwa Warumi na alikuwa na ujeuri mwingi na kuchezea mali na kuwaua watu. Alikuwa na kipote cha walinganizi (ma-Du‘aat) wake waliokuwa wakifanya kazi ya kuwapoteza watu kwa uwezo wao wote. Wao walikuwa wakiwaambia baadhi ya watu: “Huyo ni Mahdi mtoto wa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na dalili (huja) ya Allaah kwa
@jumayussuf349
7 жыл бұрын
masha alla jazaka llahu lkher
@hamisishabani4072
3 жыл бұрын
MAA SHAA ALLAH!!! SHEIKH WETU SHEIKH OTHMANI MAALIM.ALLAH AMEKUPA ELIMU,BUSARA NA HEKIMA,UANAJUA NAMNA YA KUSAFISHA MAZINGIRA YA KIELIMU YANAYOHARIBIWA NA MASHEIKH WENYE UCHACHE WA ELIMU NA AMBAO WATUPOTOSHA AMBAO HATUJAFIKIA KIWANGO CHA ELIMU NDOGO WALIYONAYO WAO.NA NDIO WAMEPOTOSHA BAADHI YA JAMII YA KIISLAM KUYAFANYA MAMBO YA KHEIRI,KAMA MAULIDI,KHITMA KUWAOMBEA DUA WAZAZI WETU NA NDUGU ZETU WAISLAM,NA MENGINEYO. JAMANI TUMSHUKURU ALLAH,KWA KUTUJAALIA KUWA NA MASHEIKH WENYE ELIMU,HEKIMA NA BUSARA KAMA ALIYOKUWA NAYO SHEIKH WETU OTHMANI MAALIM.TUNAKUOMBA YA ALLAH UMZIDISHIE KHEIRI NYINGI SHEIKH OTHMANI MAALIM PAMOJA NA MASHEIKH WETU WOTE WENYE KUSIMAMIA NA KUTUHIMIZA KATIKA MATENDO YA KHEIRI KWA AJILI YA ALLAH. AMIIN!!! ALHAMDULILLAH,SHUKRAN SANA SHEIKH OTHMANI MAALIM ALLAH UKUPE UMRI WENYE KHEIRI NYINGI NA MANUFAA KWA UMMA WETU WA KIISLAM NA WALIMWENGU WOTE KWA UJUMLA. SHUKRAN SHEIKH,ASSALAAM ALAYKUM WARAHMATULLAH.
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
Na amesema tena al-Maqriiziy katika maudhui nyengine: “Shughuli za Mawlid ya Mtume mtukufu (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) zilikuwa zikifanyika rasmi kama desturi yake katika mwezi wa Rabi’ul Awwal”. Kila mmoja anatakiwa azingatie jinsi gani Mawlid yalivyoanzishwa pamoja na uzushi mkubwa mfano: Uzushi wa kukataa na kuchupa mipaka juu ya familia ya Mtume kwa kusimamisha mawlid ya ‘Aliy, Faatwimah, Hasan na Husayn. Uzushi wa kusherehekea Idi ya Nayruuz, na Idi ya Ghatas na kuzaliwa kwa Masihi nazo ni Idi za Wakristo. Amesema Ibn Turkumani kuhusu hizi Idi za Wakristo: “Na miongoni mwa uzushi inayoleta hizaya ni wanaofanya Waislamu katika siku ya Nayruuz ya Kikristo na misimu yao mengine na siku kuu ('Iyd) kwa kupeana chakula kwa wingi. Na sadaka ya chakula isiyokubalika itarudi kwa mwenye kutoa kwa haraka au baadae. Na kwa uchache wa tawfiki na kufaulu ni yale wanayofanya Waislamu waovu kwa inayotambuliwa kama siku ya mazazi (yaani kuzaliwa kwa Yesu)” (Al-Lam‘i Fil Hawaadith wal Bid’ah, Mj. 1, uk. 293 - 316). Na imenukuliwa kutoka kwa wanavyuoni wa Hanafiyyah kwamba yeyote ambaye atafanya mambo yaliyotangulia atakuwa kafiri mfano wao (hao Wakristo). Na wakataja idadi za Idi kadhaa za Wakristo ambao Waislamu walio wajinga wanashiriki, na jinsi zilivyo uharamu wake katika Kitabu na Sunnah na yale misingi ya kisheria yaliyo kamili.
@youssouphsalum786
2 жыл бұрын
Hekma masha Allah
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
Kumpenda iwe zaidi kuliko hata nafsi zetu kama walivyompenda Maswahaba - 'Umar ilipoteremka aayah: “Nabii ni bora zaidi kwa Waumini kuliko nafsi zao” (33:6). Alisema “Ewe Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), hakika wewe ni kipenzi kwangu kuliko chochote isipokuwa nafsi yangu” Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: “Bado ewe ‘Umar! Mpaka niwe ni mwenye kupendwa zaidi kwako kuliko nafsi yako”. 'Umar (Radhwiya Allaahu ‘anhu) akasema: “Ewe Mtume wa Allaah sasa wewe ni kipenzi kwangu kuliko chochote hata kuliko nafsi yangu”. Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: “Sasa ewe ‘Umar”. Maana yake ni kuwa sasa umefikia ile daraja ya kunipenda. Kuhusu aayah hii Al Bukhaariy amehadithia kuwa Abu Hurayrah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kasema kuwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kasema: “Hakuna Muumini yeyote isipokuwa mimi ni wa kupatiwa kipa umbele kwa watu duniani na Akhera. Someni mkitaka: “Nabii ni bora zaidi kwa Waumini kuliko nafsi zao” (33:6). Sisi hatuwezi kufikia kiasi cha mapenzi ya Maswahaba waliokuwa nayo na kujitolea mhanga kwa roho zao, watu wao, mali zao, n.k. Visa vingi vipo vya kusisimua mwili vinavyothibitisha mapenzi yao kwake mfano kisa cha Khabbaab bin al-Aratt, Khubayb, Umm ‘Ammaarah Nusaybah bint Ka‘ab, Zayd, Bilaal bin Rabaah, Zu
@fahmisaid8998
4 жыл бұрын
Kama Una elmu sana siuende ukatoe khutba kwa mawahabi wenzio maana naona unaumia roho Sana sheikh mawlid sio Bida kila mkiyapinga ndio yaziddi kunawir
@abdullaalzeiby9011
6 жыл бұрын
Sheikhe ana elimu ana lugha na fikira njema lakini twamlaumu kuwa maneno mengi juu ya jambo hili hakuyasema wala hakuyataja. Zamani alkuwa hatowi rai wadhih kama hivi. Suala ambalo latufaidia sisi ummatulmuslimeen ni kujuwa hii maulidi ni ibada au si ibada? Na ikiwa ni ibada ambayo twaisoma misikitini ..jee mtume salla allahu allaihi wassallam alikuwa akijua au la ...na mbona hakutuleteya kwa wazi kama alivyotufikishiya mambo yote ya dini ..au nini kikwetu hichi ni kizuri na mungu na mtume hawajui. Mambo mengi katika hutbah yake yanashangaza na yatake yazingatiwe. Kama mambo ya shirki na owongo yaliomo katika vitabu hivyo na buradah hakuyataja wala mambo ya kupiga ngoma na kupanda na kushuka na kutuzana pesa shekhe hakuyataja kabisa ...sisi waislaamu hupata taabu kujuwa mamba ikiwa shekhe hatochukwa maudhui kamil kwani yeye hakukubaliyana na yote ya maulid. Alileta jambo mmoja tu la itraa na ambalo watu wa maulidi walilifanya jambo kubwa kwa hata kufika katika shirk kama yaliomo katika burda na makasida ambayo yamtaja ali alhabshi na sayidtna khadija hata wengine kufikakumtaja sayyidna hussein ...maulidi alrasool kutokana na seera za mtume ni kitu kizuri saana lakini bila mambo mengineyo na bila kutiya tarekhe ya kuzaliwa kwani tarekhe haijulikani ...tarekhe ya kifo chake chajulikana.. watu wakipinga huwa sio wahalilisha au watowa fatwa huwa shekhe hakueleza kama amesoma akaona maneno hayo hayana shirki wala haya itraa ya kiharamu. wallahu aalam
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwa siku hamsini na tano, kama wanavyothibitisha wanavyuoni wengi. Nayo inawafiki mwisho wa mwezi wa Februari au mwanzo wa Machi mwaka 571 BI” (Al- Mustafa, nakala ya Ansaar Muslim Youth Organisation, 1993, uk. 11). Kutokana na mapokezi hayo mawili tunaweza kuiweka tarehe ya kuzaliwa kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) baina ya tarehe 25 Swafar na tarehe 25 Rabiy’ul Awwal na Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anajua zaidi. ‘Afiyf ‘Abdul-Fattaah at-Twabbarah na Abul Hasan ‘Ali Nadwi wamesema katika vitabu vyao kuwa: “Aminah alizaa alfajiri siku ya Jumatatu tarehe 9 au 12 ya Rabiul Awwal, mwaka wa ndovu. Mahmuud Pasha, maarufu kutoka Misri, amefanya hesabu ya tarehe ya kuzaliwa na kupata kuwa ni Jumatatu tarehe 20 Aprili mwaka 571 BI, inayokwenda sambamba na tarehe 9 Rabiul Awwal” (Ma‘al Ambiyaa Fil Qur-aanl Kariym, uk. 338 na Muhammad RasulluLlah, uk. 91). Inaonekana kuwa wanavyuoni na wana-historia wa wakati huu wamechukua tarehe 9 ya Rabi’ul Awwal kuwa ndiyo aliyozaliwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) {Allamah Shibli Nu‘mani, Seeratun Nabi na Prof.
@issatarimo364
4 жыл бұрын
Acheni Mambo yenu bidaa wap?
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
Ya Kwanza: Jambo hili halikufanywa na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wala hakuamrisha lifanywe wala hawakufanya Maswahaba (Radhwiya Allaahu ‘anhum) wala hata mmoja miongoni mwa Tabi‘iyna wala waliowafuata wala hawakufanya Waislamu katika zama zilizokuwa bora za mwanzo. Na hizi zilikuwa ni zile karne tatu za mwanzo kuanzia Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) mpaka mwaka 300 Hijri. Jambo hili lilianzishwa na watu kama tulivyotangulia kueleza waliokuwa karibu na ukafiri kuliko Imani nao ni Baatwiniyyuun na baada ya karne hizi tatu bora. Jambo hili likifanywa kwa kukaririwa ni kwamba yule mwenye kufanya anaingia katika adhabu kali aliyoahidi Allaah Aliyetukuka kwa mwenye kufanya. Allaah Anasema: "Na atakayemuasi Mtume baada ya kumdhihirikia uongofu na akafuata njia isiyokuwa ya Waumini, Tutamgeuza alikogeukia mwenyewe na Tutamwingiza katika Jahannam; napo ni pahali pabaya kabisa pa mtu kurudia”(4:115). Hivyo, yule anayefanya Mawlid bila shaka hafuati njia ya Waumini miongoni mwa Maswahaba, Tabi‘iyna na wanaowafuatia. Ya Pili: Mwenye kufanya amali hii anaingia katika yale aliyoyatahadharisha Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) pale aliposema:
@user-qe8xp6ii1u
3 жыл бұрын
Kwanz Hata Usomaji wako M bovu,Huwez tamka Vzr,halaf hayo maneno yako ni mwanachuon gani Alokuwleza hivyo!? pia sis Ahlu sunna tunapo mahala pa kurudi na kuwasikiliza Salaf wameielewaje hadith hii. Ibn masoud Anasema"Fuateni wala msizushe... Ibn Omar anasema"Kila Bidaa ni upotevu Hata kasma watu wataona bidaa Hiyo ni nzr.. Pia Imaam malik anasema Amenukuliwa ktk Kitab Cha Al imaam Shaatwibiyy kiitwacho Al iitwisaam"Yeyote mweny kuzusha Bidaa ktk uislam,Atakuwa amedai kuwa Mtume Mohammad amefany khiyana ya Risala yake..Kwa sabab Allah anasema"Hiv leo nimekukamilishien Din yenu na nikatimiz neema yang Kwenu,Nanimeridhia Uslam Ni Dini Kwenu..Basi Jambo lolote Ambalohalikuwa Dini Siku hiyo Haliwez kuwa Nini Leo." Hayo yote Yanasimanga Bidaa zote Na Pia waanachuon wameandik Vtab vingi Sana ktk Mlango huu mfno"Al amru bil ittibaaa'a wannahyu anibtidaab cha Al imaam Suyjutiyy Ambaye ni Shafiyiyy... Ila wew Unasimama Unawaongopea watu,Unadhidharau juhud Zote walizofany wanachuoni??Hakika wew ni jaaahil kabisaaa
@sabraham5308
5 жыл бұрын
Asalam aleikum, kuna sheikh anaemfikia Sheikh Abdullah Saleh Farsy,ni mtu wa mwanzo aliyeutafsiri msahafu kwa kiswahili,na akatuasa makosa mengi yaliyokuwemo ndani ya kitabu cha maulidi ya barzanje,lea ufupi aliyapinga,kwa hugo maneno mazuri ya kupanga na kuvutia, hayatohalalisha barzanje, kwa kuwa kimeandikwa kiarabu,na yeye anajaribu kuleta ufasaha wa kiarabu kwa hawaa zake, mfano mdogo tu,maulamaa wa makkah muharram na madina munawari, hawakubaliani ma maulidi na ni marufuku,ni Bora kama ana ufahamu huo ,angekwenda huko kuwafundisha yale aliyoyaona yeye yanafaa,tuone itakuaje, lakini hilo hathubutu na wala hatothubutu,ataishia humu humu vijiweni,na yeye anajua hilo,huko ikiwa kiarabu basi huko atatolewa ngozi walizokuwa masahaba wa mtume wakiandika,asalam aleikum.
@mwanamisipofu3212
8 жыл бұрын
Mashallah
@twalibfaqih9385
Жыл бұрын
Tusomeni maulid ni uzushi hakuna kitu icho kabisa
@ibrahimabdillah5729
5 жыл бұрын
Njaa mbaya sana We endelea kula tu pesa za mabosi zako
@Kekulebenzene
5 жыл бұрын
Hata maana ya bidaa haijui, eti kila asichofanya mtume (saw) ni bidaa
@ahmadsalim4417
4 жыл бұрын
@@Kekulebenzene kumbe ww una bidaa yko????
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
Sunnah wala Ijma’a wala Qiyaas inayoonyesha usahihi wa jambo hilo. Na hakuna pia hata dalili ya kiakili wala kimaumbile, na jambo lolote linalokuja kwa njia hii basi huwa ni uzushi muovu usiotakiwa katika Dini. Amesema al-Haafidh Ibn Rajab: “Na asili ya Bid‘ah ni ile inayozuliwa na isiyokuwa na asili katika sheria inayokuwa ni dalili kwayo” (Jaami‘ul-‘Uluum wal Hikam, Mj. 2, uk. 127). Na amesema tena: “Na chochote kinachozuliwa na yeyote na kisha kikinasibishwa na Dini na kikawa hakina asli (misingi) katika Dini atarudishiwa mwenyewe. Huo utakuwa ni upotevu na Dini ipo mbali na kitu hicho. Ni sawa ikiwa hilo limefungana na mambo ya ki-itikadi au amali (matendo) au kauli zilizo wazi na zilizofichika” (Jaami‘ul-‘Uluum wal Hikam, Mj. 2, uk. 128). Bid‘ah katika lugha ni “Kila lenye kuzuka (uzushi)” na katika sheria ya Kiislamu ni “kuzuka kitu katika Dini baada ya kukamilika” (yaani baada ya mafunzo ya Mtume [Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wasallam]) {Shaykh Said Musa, Majadiliano Juu ya Mawlid, Chapa ya Kwanza, 1985, Dar es Salaam, uk. 1}. Ufisadi na uharibifu wa kuruhusu jambo hili upo wazi kabisa, na hapa tunanukuuu baadhi ya nukta katika mas-ala hayo. Nayo ni kama yafuatayo:
@user-ql2om7qj3v
5 жыл бұрын
Mashaallah maneno yako uko sawa
@mustayoo
5 жыл бұрын
Hizo faida mtume hajaziona ukaja kuziona ww?
@meena-ol6fo
4 жыл бұрын
Kwenda zako wewe nyie ndio mnaopotosha watu
@muhidinali8180
3 жыл бұрын
Wazushiwengi wanawafurahia mashekhe wakizushi eti sikuhizi kuna mashekhewengisana yani hatanyinyi mnajifanya mnajua kuliko mtume s a w pia mnayoyafanya mengì ktka dini maswahaba ambao ndio wanafunzi wa mtume s a w hawakufanya maana sikatika dini ilala nyinyi mna yatetea hadidthi imesha shereheshwa na maulama turudietu ktka vitabu tusipambepambe ktka wanachuoni waloisherehesha hadithihii ni imam ibnu rajabul hambaly imam shatwibi ktka iitswam nawengineo
@abdulsamadkhalfan4075
10 жыл бұрын
MASHALLAH
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
Suala la sisi kujiuliza ni kuwa; Je, haya Mawlid yalianza lini? Jawabu ya suala hili kwa mwanachuoni wa Ki-Sunnah, Al-Imaam al-Maqriiziyni: “Katika kipindi cha uongozi wa Faatwimiyyuun (hawa walikuwa ni Rawaafidh (Mashia) katika kipote cha Ismailiyyah [Makoja] katika nchi ya Misri) walikuwa wanachukuwa hii ni misimu ya sherehe ambapo walikuwa wakiwakunjulia hali za raia zao na kuwakithirishia neema. Na walikuwa hawa watawala wa Faatwimiyyuun katika mwaka mzima wana misimu ya sherehe na Idi zao nazo ni kama zifuatazo: Msimu wa kichwa cha mwaka, Msimu wa mwanzo wa mwaka, Sherehe za ‘Aashuraa, na Mawlid ya Nabii (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), na Mawlid ya ‘Aliy bin Abi Twaalib (Radhwiya Allaahu ‘anhu), na Mawlid ya Hasan na Husayn (Radhwiya Allaahu ‘anhuma), na Mawlid ya Faatwimah az-Zahraa (Radhwiya Allaahu ‘anha), na Mawlid ya kiongozi wao aliye hai kwa wakati ule, usiku wa kwanza wa Rajab, na usiku wa kati ya Rajab, na Mawlid ya usiku wa Ramadhaan na mwisho wa Ramadhaan na Msimu wa 'Iydul Fitwr na Msimu wa 'Iydul Adh-ha na Idi ya Ghaadir, Msimu wa ufunguzi wa Ghuba na Siku ya Nairuuz na Siku ya Ghatas na Siku ya Mazazi, na Siku ya Vipandio, Kis-wa (nguo) ya Msimu wa Kusi na Kaskazi, Alhamisi ya Adasi na Siku ya Ubatizo” (Al-Khutwat, Mj. 1, uk. 490 na baada yake). na amesema tena katika kitabu chengine: “Na katika mwezi wa Rabi’ul Awwal walijilazimisha watu kuwasha kandili usiku katika njia zote na vichochoro vyake huko Misri”.
@mohameddara839
3 жыл бұрын
Mashaa Allah
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
‘Abdul-Hameed Siddiqi, The Life of the Prophet}. Hekima ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Kuificha siku hiyo ya kuzaliwa kwake Anaijua Yeye mwenyewe. Hivi sasa watu wamevuka mipaka katika kuisherehekea siku na mwezi huo na bado kuna tofauti kwa siku ya kuzaliwa kwake. Jambo ambalo linajulikana kwa uhakika bila ya utata wowote ni siku aliyozaliwa, kwani haya aliyasema kwa kauli ambayo haina maana mbili. Imepokewa kwa Abu Qataadah (Radhwiya Allaahu ‘anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliulizwa juu ya kufunga (Swawm) ya Jumatatu. Akasema: “Hiyo ilikuwa ni siku niliyozaliwa na ndio siku niliyopatiwa Utume au niliyoteremshiwa Wahyi” (Muslim). Na ili tuwe tumemfuata vilivyo Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) katika Sunnah zake inatakiwa tuwe tunafunga siku ya Jumatatu kila wiki na jambo hilo litakuwa linatukaribisha kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala). 4.0 KUBAINISHA HUKUMU YA MAWLID Jueni, Allaah Aturehemu sote ya kwamba Mawlid ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) hayapo katika sheria na hakuna dalili katika Kitabu wala
@hasanisaidishabani3879
2 жыл бұрын
Shekh kaelezea vzr unatakiwa ili umuelewe kwanz uondoe akili yakujifany unajua tuliza akili utamuelewa sanaa muda mwengine ukisikiliza kwakubishana utoelewa ila shekh kapita ktk mipito ya kiufundii sanaa tenaaa sanaaa
@mikekhalifaali7510
Жыл бұрын
Maulid ni upuuz
@sulaymansulayman4284
10 жыл бұрын
Kosa kubwa pia baadhi ya maneno katika Maulidi yana kufru ya kumpandisha Mtume صلى الله عليه وآله وسلم cheo cha usawa na Allaah سبحانه وتعالى wakati yeye ametuonya tusifanye hivyo ((Msinitukuze Kama Manaswara walivyomtukuza Masiyh mwana wa Maryam, hakika mimi na mja kwa hiyo semeni mja wa Allaah na Mjumbe Wake)) [Al-Bukhaariy na Muslim] SHUKRAN NDUGU ZANGU Nakupendeni kwa ajili ya Allah Abu Abdir-Rahman UK
@omarjomar6670
7 жыл бұрын
wapi mtume alipopewa darja ya uungu katk jambo gani
@yaziduiddi481
6 жыл бұрын
ssyy ss ww kasome huna unachokijua ktk maulid unaijua kufru ww au unajiropokea tu
@aliyomar9140
5 жыл бұрын
yazidu iddi maulid tutasomaaaa pasukeniiii na mawahabi wenzenu
@ahmadsalim4417
4 жыл бұрын
Lkn ingekua nivyema ukatubainishia niwap mtume alitukuzwa nakupewa cfa za Allaah sio unaropokatu
@sabraham5308
4 жыл бұрын
Wacha kupotosha Maalim.
@kherysalum638
4 жыл бұрын
Omba mnakasha sio kuongelea kwenye majukwaa
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
aalihi wa sallam) na kumfuata kwa kila jambo, kwa wazi na siri. Inabidi pia tujiondoshe na ule ufahamu finyu wa kuwa kumpenda Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ni kucheza na kupiga ngoma wakati na siku maalumu katika mwaka. Na wale wanaotekeleza jambo hilo wanasema ya kwamba hiyo ndio dalili ya wazi kuwa wao wanampenda Mtume (tujiondoshe na ule ufahamu finyu wa kuwa kumpenda Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na yeyote asiyefanya hayo basi anamchukiza na hivyo kuchukiwa na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Na jambo hili bila shaka ni kuipindua ile maana ya mapenzi kwa Allaah na Mtume Wake, kwani mapenzi kwa Allaah na Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) lazima yawe ni katika kufuata Sunnah zake zote. Kumpenda Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ni kufuata zaidi sunnah zake kuliko kumsifu sana kama Anavyosema Allaah: “Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Allaah basi nifuateni mimi, Allaah Atakupendeni na Atakufutieni madhambi yenu. Na Allaah ni Mwenye Kufuta madhambi na Mwenye Kurehemu” (3:31). Kumpenda sio kumkumbuka kwa kumsifu mara moja kwa mwaka tena kwa njia isio sawa bali kila siku na kumsifu bila kufuata Sunnah zake hakuna faida wala thawabu.
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
Yule mwenye kufanya mahaba kwa Mtume ni kufanya haya Mawlid anabadilisha sheria ya Allaah ambayo inasema kuwa mapenzi sahihi inakuwa ni katika kumfuata Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Bali hii ndio ile hakika ya mapenzi ambayo yamleta mtu karibu na Allaah na kumjaalia yeye atoke katika zile ada za kufananisha na yale wafanyao Wakristo katika sikukuu zao. Na kwa hili tunaelewa ya kwamba: “Haihuishwi (haifanywi) Bid‘ah isipokuwa huondoka Sunnah miongoni mwa Sunnah madhubuti”. Ya Nane: Haya Mawlid yanafanana kwa uwazi kabisa na Dini ya Ukristo, ambayo wafuasi wake wanasherehekea mazazi ya Masihi ('Iysa). Na hakika ni kuwa sisi tumekatazwa kushabihiana na wao kama alivyosema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Na yeyote mwenye kushabihiana na watu yu pamoja nao” (Iqtidhaa’ as-Swiratwil Mustaqiym ya Ibn Taymiyyah, Mj. 2, uk. 581). Ya Tisa: Ni maalumu na yenye kueleweka kwa kila mmoja ya kwamba Maswahaba ndio waliokuwa wakimpenda zaidi Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kuliko wanadamu wengine kwa ujumla na Waislamu wengine hasa katika wale waliokuja baada yao. Lakini watu ambao wanafanya bid‘ah hii ya Mawlid wanasema kinyume ya hayo kwamba wale wasiosoma na kushirikiana nao huwa hawampendi Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Na hii ni tuhma kubwa kwa watu ambao walijitolea mhanga katika kumhami Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), kutekeleza
@mohagurey2214
3 жыл бұрын
Hio bid'a itakufa pole pole bi'idnillahi ta'ala.
@sulaymansulayman4284
10 жыл бұрын
Watu huwa tunasema haya mambo tumerithi kwa wazee na masheikhe wetu, ina maana wao hawana Elimu nyie masheikhe wa internet ndo mlosoma, Allah anajibu hili kwa kusema سبحانه وتعالى: (Na wanapoambiwa: Njooni kwenye yale Aliyoyateremsha Allaah, na kwa Mtume, husema: Yanatutosha tuliyowakuta nayo baba zetu. Je, hata ikiwa baba zao walikuwa hawajui kitu wala hawakuongoka?)) [Al-Maaidah: 104]
@abdiamiri8041
2 жыл бұрын
Twayb
@sabraham5308
4 жыл бұрын
Akikipenda mtu kitu,basi lazima akilazimishe,maulidi ni ibada?
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
miaka mingi sana. (Tafsiri ya Mawlid BARZANJI - KADHI SHEIKH ABDULLA SALEH FARSY, ZANZIBAR, Uk.(iv) ) 3.0 MAZAZI YA MTUME (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) Ni maarufu kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alizaliwa baada ya kuaga dunia babake. Lakini wana-taariykh wametofautiana kuhusu mwaka na mwezi aliozaliwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Safi-ur-Rahmaan Mubarakpuri, mwanachuoni aliyepata zawadi ya kwanza katika mashindano ya kuandika historia ya Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ameandika yafuatayo katika kitabu chake: “Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), bwana wa Mitume, alizaliwa katika mtaa wa Bani Haashim katika mji wa Makkah, Jumatatu, tarehe 9 Rabi’ul Awwal, mwaka ule ule wa ndovu na miaka arobaini baada ya utawala wa Kisra (Khsru Nushirwan) yaani tarehe 20 au 22 Aprili 571 BI (Baada ya kuzaliwa ‘Iysa), kulingana na alivyohakikisha mwanachuoni mkubwa Muhammad Sulayman al- Mansourpuri na mwana-falaki Mahmud Pasha” (Ar-Rahiyqul Makhtuum, uk. 62). Sirajur Rahmaan katika kitabu chake amesema: “Tukio hili la ndovu lilitokea mwezi wa Muharram kabla ya kuzaliwa kwa Mtume
@user-ql2om7qj3v
5 жыл бұрын
Sheikh nimekusikiza vizuri sana kumbe hata wewe mtupu kabisa.hata siwezi sikiza tena durus zako.hufai
@nurdinmohamed1050
5 жыл бұрын
Shekh huna adabu hakuna mtu perfect
@bobsule4036
4 жыл бұрын
Shekh makosa ww nenda ukasome usijisemee
@wamsalsuyuwtwiy9229
3 жыл бұрын
Kuwa na adab ya mazungumzo
@abubakarnassor8280
3 жыл бұрын
😋
@johrahali583
5 жыл бұрын
Bidaa ni aina mbili....katika dalili ya Quran na sunnah....
@rizikiali8173
5 жыл бұрын
nikweli sheikh
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
Maulid ni Bidaa ibn Taymiyyah amwzungumza hayakufanywa na maswahaba kwani hao ndio waliompenda mtume s.a.w na haikuwepo ya kuwazuia iweje ww uhalalushe ubidaa uzushi katika dini Mila hii imetokana na makoja,mashia maismailiya walizitawala nchi za kisunni kwa zaidi ya miaka 270 ndio wakawaachia uzushi huuu wa mawlid Allwah anajua zaid
@shafiisaidi3305
4 жыл бұрын
Ebu kausha Bhna nenda mbele
@birdofpry3897
6 жыл бұрын
Kuna watu asili yao ni upinzani tuu hata ukiwafahamisha hawaelewi sheikh wetu
@aliyomar9140
5 жыл бұрын
Maimona Bakar walah ni kwelii.
@sabraham5308
4 жыл бұрын
Sasa ina maana wale wanyoingoza dini makka Al qubra na madinat al munawari,maktaba al elmu ya waislamu,wanakosea wakiyapinga maulidi,makaka na madina maulidi marufuku,sheikh unayo ya kuwaambia. Hivyo sheikh elmu yako umewazidi maulamaa wakubwa wa makka na madina lmunawari,hiyo elmu yako umeitoa wapi,utawadang'anya hao waliopumbaa.
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
isipokuwa Mnafiki. Kwa hiyo Allaah Atampenda anayewapenda na Kuwachukia anayewachukia” (Al- Bukhaariy na Muslim). Hawa Maswahaba wa ki-Answari hawangependwa na Allaah isipokuwa wao walikuwa msitari wa mbele katika kumpenda na kumfuata Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), kwani Allaah Amesema hilo na unaweza kuirudia aya ya 31 ya Suratul ‘Imraan tuliyotangulia kuitaja. Twabaan Maswahaba wa Ki-Muhajirina pia wapo katika aayah tulizozitaja pamoja na Hadiyth nyingi ambazo hatukuzinukuu hapa. Ya Kumi: Hakika mwenye kufanya haya Mawlid ameingia katika yale aliyoyakataza Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kwa uwazi kabisa. Amesema Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Msinitukuze kama Manaswara walivyomtukuza 'Iysa mwana wa Maryam. Kwa hakika mimi ni mja, hivyo semeni: Mja wa Allaah na Mjumbe Wake” (Al-Bukhaariy). Hakika amekataza Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kumtukuza na kumsifu kupita kiasi sifa ambazo zinapindukia kwani hilo ndilo lililowafanya Manaswara kupotea katika njia ya haki. Na katika hayo ni kukataa kuitwa hata “Khayrul Bariyyah (Mbora wa viumbe)”. Na inatosha kumuitaRasullullah (Mjumbe wa Allaah) kama alivyoitwa na mwenyewe Allaah au walivyokuwa wakimuita Maswahaba zake.
@johrahali583
5 жыл бұрын
Wallai kumbe huyu ni sheikh mtupu mwenye story
@Kekulebenzene
5 жыл бұрын
Johrah Ali anaacha kauli za wanawachuoni eg imam malik kuhusu bidaa analeta stori et simba😁😁😁
@alisalum6330
5 жыл бұрын
Mbaya zaid mmewafanya waislam waamin hio ni moja ktk ibada. Tushikamane na sunna zake na maswahaba ktk kila kitu huko ndiko kumpenda si maulid hii ni dini ya hoja msitumie akili zenu kwa kupotosha umma.
@majidsaid08
5 жыл бұрын
wewe hoja yako ni ipi???
@johrahali583
5 жыл бұрын
Heheheheh zuzuzu sanaaa bidaa nzuri na mbaya toa dalili si story tu?
@Safinatulshifaa
5 жыл бұрын
hawa wasichana ndio walikuwa wanapata fursa ya kukutana na wapenzi wao. Wengi wetu tumeyashuhudia hayo katika miaka ya sitini na kabla ya hapo na baada ya hapo mpaka katika miaka ya sabiini waalimu waliokuwa wakitoka Lamu kwenda kusoma Mawlid katika visiwa na vitongoji vyengine. Mambo ambayo yalikuwa yakitendwa na kutendeka ni kinyume kabisa na Uislamu na madhambi makubwa zaidi yakifanywa na wanavyuoni. Kwa sababu ya ujinga katika Dini hawa mabwana walikuwa wanazini na mabibi wa watu na kupatiwa kama tunu wasichana mabikra wawe ni wenye kulala nao kwa hoja kuwa kitovu cha mwalimu kikigusana na kitovu cha msichana au mwanamke basi msichana au mwanamke yule hataingia Motoni. Allaah Atuepushie na Atuongoze katika yaliyo ya sawa. Itakuwaje matendo mabaya yote haya yawe ni katika kujikurubisha na Allaah Aliyetukuka. Upotofu ulioje katika mambo haya yanayofanywa kwa kisingizio cha Dini. Ya Kumi na Tano: Kufanywa na kujumlisha mambo ya kufuja na kupoteza mali kwa watu wasiostahiki kabisa. Na Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Ametukataza kufuja mali wala kuwa mabakhili kwani hizo si sifa za Waumini. Anasema: “Na wale ambao wanapotumia hawatumii kwa fujo wala hawafanyi ubakhili, bali wanakuwa katikati baina ya hayo”(25:67).
@khalfansharji9790
5 жыл бұрын
Waisilamu wanakuelewa sheikh ila siyo mawahabi!!! Kwani hata hayo mambo ya karne tatu baada ya rasuli si khabari za mawahabi?Ogopa sana fitna ya najdi ni balaa kubwa katika umma.
@bachochosalimu9015
4 жыл бұрын
Je ninani Alie kusanya quruan kwa kuiweka kwenye vitabu je alikuwepo wakati wa mtume au baada ya kufa mtume je sinijambo la kheri basi yatosha maulidi kuwa ni heri
Пікірлер: 206