Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Peter Serukamba ameagiza kumfuta kazi fundi anayejenga madarasa katika shule ya Sekondari ya wasichana Lugalo na shule ya Ikokoto kwa kutokamilisha miradi kwa wakati huku akimuagiza afisa manunuzi kumwondoa mmoja wa wazabuni kwa kuchelewesha vifaa vya ujenzi kwenye miradi ya Halmashauri ya Wilaya Kilolo.
Hayo yamejiri leo septemba 19,2024 wakati alipofanya ziara ya kutembelea na kukagua miradi ya ujenzi wa shule ambapo awali alianza kukagua katika shule ya sekondari ya Ifingo ambapo alikuta mradi bado haujakamilika na vifaa bado havijafika katika eneo hilo na baadae alifika katika shule ya Sekondari Kilolo ambapo huko alikutana na tatizo la kutokuwepo kwa vifaa vya ujenzi
lakini alipofika katika Shule ya Wasichana ya Lugalo napo huko akakutana na kisa kingine ambapo fundi Ndg.Godwin Mshana aliyepewa kazi ya ukamilishaji wa madarasa kasi ya utendaji kazi yake kusuasua ambapo Mhe.Serukamba amemwagiza Mkurugenzi Tarehe 26 mwezi huu kama atakuwa hajafikisha majengo kwenye lenta basi afutwe kazi apewe kazi mtu mwingine huku akimfuta kazi fundi huyo kutoendelea na ujenzi katika shule ya Ikokoto
Pia Mhe Serukamba ameagiza kumondoa Mzalendo ambaye ni mmoja wa wazabuni kwa kushuindwa kupeleka vifaa kwa wakati na kupelekea ujenzi kusuasua na kuagiza kumuweka mzabuni mwingine ambaye ni CF.
sambamba na hayo Mhe. Serukamba ameendelea kuwahimiza watendji na wataalamu kusimamia miradi na fedha zilizotolewa na Serikali ya awamu ya sita ili iweze kuisha kwa wakati
Негізгі бет RC: SERUKAMBA AMKALIA KOONI MZABUNI, FUNDI NA AFISA MANUNUZI-KILOLO
Пікірлер