Sema Na Roho Yangu | Nyimbo za Mungu 243 | Tabernacle de Kolwezi
1.
Sema na roho yangu, Bwana, na pendo kubwa;
Uniambie wazi: “Sitakuacha pekee.”
Moyo ufunguliwe kwa kusikia neno,
Na unijaze roho na pendo, sifa kwako.
Chorus
Sema na roho yangu, Bwana, na pendo kubwa;
Uniambie wazi: “Sitakuacha pekee.”
Sasa tayari mimi kukusikia, Bwana:
“Utashindishwa nami, na utakuwa huru.”
2.
Sema na wana wako kuwaonyesha njia,
Na unijaze tele na shangwe na furaha,
Ili watoe roho kutumikia Mungu
Hata kurudi kwako kwa kuwatwaa mbinguni.
3.
Kama ulivyoonyesha njia yako zamani,
Uniyafahamishe mapenzi yako kwami;
Uniongoze jinsi kukutukuza, Bwana,
Hata maneno yako nitayatii daima.
Dimanche 26 Juin 2016 Tabernacle de Kolwezi
Nyimbo za Mungu 243
#Maranatha
Негізгі бет Sema Na Roho Yangu | Nyimbo za Mungu 243 | Tabernacle de Kolwezi
Пікірлер