Mwanamke aliyejitambulisha kwa jina la Havinitoshi amejikuta akimiminiwa ‘noti’ za fedha bila kutarajia baada ya kueleza mbele ya Rais Magufuli kero yake inayohusu manyanyaso wanayopata wafanyabiashara ndogondogo mjini Morogoro.
Tukio hilo limetokea wakati Rais Magufuli akihutubia baada ya kuzindua kiwanda cha sigara cha Philip & Morris kilichoko Morogoro.
Baada ya kusikiliza kero yake, Rais Magufuli alitoa agizo kwa mamlaka kuwaacha wafanyabiashara hao wafanye biashara zao bila usumbufu.
Pia Rais Magufuli aliamua kumchangia mama huyo shilingi laki moja baada ya kueleza kuwa aliwahi kupigwa faini baada ya kukamatwa akifanya biashara katika eneo la stand.
Tazama ilivyokuwa.
Негізгі бет Tazama Rais Magufuli 'alivyomjaza fedha' Bibi Havintishi wakati akihutubia
Пікірлер: 345