Na.Elimu ya Afya kwa Umma.
Katika kukabiliana na Ugonjwa wa Marburg ulioripotiwa hivi karibuni mkoani Kagera, Serikali kupitia Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais TAMISEMI, Ofisi ya Waziri Mkuu, Wizara zingine za Kisekta pamoja na Wadau mbalimbali inaendelea kutekeleza mikakati ya uelimishaji na uhamasishaji jamii ikiwa ni pamoja na kuwajengea uwezo Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii 1,322 katika Mitaa, Vijiji na Vitongoji vyote vya Halmashauri ya Bukoba Vijijini na Manispaa ya Bukoba.
Hayo yamebainishwa leo April 8, 2023 katika Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera na Kaimu Mkurugenzi Msaidizi Sehemu ya Elimu ya Afya kwa Umma Wizara ya Afya Dkt. Tumaini Haonga wakati akizungumza katika mwendelezo wa utoaji wa elimu ya afya kuhusu kinga na tahadhari dhidi ya Ugonjwa huo.
“Kupitia Sehemu ya Elimu ya Afya kwa Umma, Serikali imetekeleza mikakati mbalimbali ili kuzuia ugonjwa huu usienee maeneo mengine nchini. Ili kuwafikia wananchi mahali ambapo wanapatikana, Serikali inawatumia Wahudumu wa Afya Ngazi ya Jamii kwa kuwajengea uwezo wahudumu wapatao 1322 ambapo kati yao Wahudumu wanatoka Halmashauri ya Manispaa ya Bukoba na Wahudumu wanaobaki wanatoka katika Halmashauri ya Bukoba Vijijini” amesema.
Pata elimu kuhusu masuala yote ya afya kupitia Channel hii. Mafunzo yote yanatolewa na Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto kupitia Idara ya Kinga, Kitengo Cha Elimu ya Afya kwa Umma kwa kushirikiana na wadau mbali mbali
#elimuyaafyakwaumma
Негізгі бет TAZAMA WAHUDUMU WA AFYA NGAZI YA JAMII 1,322 WAJENGEWA UWEZO KUKABILIANA NA UGONJWA WA MARBURG.
No video
Пікірлер