Katibu mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii DKT Hassan Abbas amelipongeza Jeshi la Kujenga Taifa kupitia Shirika lake la uzalishaji mali Suma JKT kwa jitihada zake za kuendelea na ujenzi wa nyumba za wananchi wanao hamia Kwa hiyari kutoka hifadhi ya Ngorongoro na kuhamia katika kijiji cha msomera Wilayani Handeni Mkoani Tanga
Hayo ameyasema wakati alipotembelea kuona maendeleo ya ujenzi nyumba hizo unaondelea katika kijijini cha Msomera.
Kwa upande wake Mkuu wa wilaya ya Handeni Mhe. Albert Msando amezishukuru Taasisi mbalimbali zinashirikiana katika ujenzi huo Kwa namna walivyo shiriki kikamilifu kutemeleza mradi huu wa ujenzi wa nyumba hizo hadi kufikia asilimia 90%.
Awali akitoa taarifa kwa Mgeni Rasmi Operashini Kamanda wa Mradi huo wa ujenzi wa nyumba 5000 msomera, Kanali Sadick Mihayo amewahakikishia wananchi wanaohamia kwenye nyumba hizo kuwa ni bora na zimejengwa kwa kiwango cha hali ya juu.
Naye Kamishna uhifadhi Ngorongoro DKT Elirehema Doriye, ameishukuru serikali ya jamhuri ya muungano Kwa kutenga Kijiji cha Msomera Kwa ajili ya wananchi wa Ngorongoro .
Ujenzi wa nyumba za Msomera mpaka sasa umefikia Asilimi 90 ambapo jumla ya nyumba
2500 kwa eneo la Msomera zitakamilika muda wowote kuanzia sasa, Huku ujenzi huo utahamia maeneo mengine ya Kitwai na Kilindi.
Негізгі бет UJENZI WA NYUMBA MSOMERA WAFIKIA ASILIMIA 90
Пікірлер