Serikali imesema inakuja na muongozo wa wanaojitolea kufanya kazi kwenye taasisi mbalimbali ambao pia utaangalia ni kwa namna gani wanaweza kulipwa.
Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, George Simbachawene katika kipindi cha maswali na majibu wakati akijibu swali la nyongeza la Mbunge wa Mbomba (CCM) Condester Sichwale
Sichwale ameuliza Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu) inaonaje kuwaandikia waraka Halmashauri ili kuwalipa wanaojitolea.
Негізгі бет Wanaojitolea kuanza kulipwa, Serikali yataja ujio wa muongozo maalumu
Пікірлер: 1