Baadhi ya wanawake wa Kata ya Lutale iliyopo wilaya ya Magu, mkoani Mwanza wamelalamikiwa na waume zao kuwa ni chanzo cha migogoro ndani ya ndoa zao.
Hayo yameelezwa katika mwalo Igombe, kata ya katale wilaya ya Magu kwenye mkutano wa hadhara ulioitishwa na Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza Naibu kamishina wa Polisi (DCP) Wilbroad Mutafungwa ikiwa ni muendelezo wa ziara ya kutembelea visiwa na maeneo yaliyopo pembezoni mwa ziwa victoria kutoa elimu ya usalama wa majini, kusikiliza kero,changamoto, malalamiko na kupata ushauri kutoka kwa wananchi.
''Unapochukua hatua flani katika lile kosa ambalo mke wako amekufanyia anakimbilia kituo cha Polisi kisha Polisi wanakukamata na kukuchukulia hatua za kisheria, lakini wanawake ndio chanzo cha matatizo kwenye ndoa'' amesema Mzee Mali Msoga.
Akizungumza na wananchi hao wa Kata ya Lutale kamanda Mutafungwa amesema jukumu la kuzuia uhalifu ni la wananchi wote hivyo, mwananchi anatakiwa ashirikiane na Jeshi la Polisi katika kuzuia vitendo vya kiharifu.
''Kubwa zaidi inatakiwa kujiepusha na matukio ya kikatili Kwa wanawake, watoto na Kwa wanaume pia nyinyi mnaokaa pembezoni mwa ziwa victoria mkiendeleza shuguli zenu, Jeshi la Polisi tunawambia utajiri unakuja Kwa kufanya kazi na sio kwa njia za kishirikina, ushirikina ni njia mojawapo ya kujitafutia umasikini" amesema kamanda Mutafungwa.
Aidha, kamanda Mutafungwa amewataka wavuvi na wananchi hao kuhakikisha wanazingatia usalama wao pindi wanapotumia mitumbwi katika kazi zao za majini Kwa kuvaa vifaa vya uokoaji ili kujiepusha na vifo vinavyoepukika pindi ajali inapotokea wakiwa ziwani.
Kwa upande wake, Koplo wa Polisi (Cpl) Stella Liymo kutoka dawati la jinsia na watoto ameiasa jamii kuacha tabia za kurusha picha za watoto waliotendewa ukatili kwani kufanya hivyo ni kuwaharibia na kufifisha ndoto zao.
Hivyo, badala ya kusambaza picha za watoto waliofanyiwa ukatili Cpl Stella amewataka wananchi hao kutoa taarifa za watoto waliofanyiwa ukatili Polisi ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi ya wahalifu.
Naye, mkuu wa Polisi wilaya ya Magu mrakibu mwandamizi wa Polisi (SSP) Makame Haji amewaomba wananchi hao kuendelea kutuo ushirikiano Kwa Jeshi la Polisi Kwa kutoa taarifa za uhalifu na wahalifu ili hatua za kisheria siweze kuchukuliwa haraka iwezekanavyo.
Негізгі бет Wanaume Wataja Wake zao Chanzo cha Migogoro kwenye ndoa.
Пікірлер