Lori la mizigo lililokuwa likitoka Dar es Salaam kwenda Burundi, limepata ajali baada ya kupinduka leo Julai 9 saa 2:00 usiku wilayani Kilosa Mkoa wa Morogoro na kisha kuwaka moto, ambapo dereva wa lori hilo anahofiwa kufariki.
Mkuu wa Wilaya ya Kilosa, Shaka Hamdu Shaka amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo, akisema chanzo cha ajali hiyo imehusisha gari dogo lililokuwa linatoka Dodoma kwenda Morogoro baada ya kuyumba na kuligonga lori hilo.
Dereva wa gari dogo imeelezwa amepelekwa hospitali kwa matibabu.
Akitoa taarifa ya awali, Shaka amesema chanzo cha ajali hiyo kimetokana na dereva wa gari ndogo kushindwa kuhimili gari lake kwenye kona kisha kugonga mti na baadaye kuparamia lori hilo na kusababisha gari hilo kutumbukia darajani.
Hata hivyo hadi sasa haijajulikana alipo dereva wa lori hilo ambaye anahofiwa kufariki dunia.
Негізгі бет #breaknews
Пікірлер: 8