Yara Tanzania tunayofuraha kuzindua huduma mpya kwa wakulima kupitia mpango wa AfricaConnect. Kwa kushirikiana na mbia mpya Jubilee Insurance @jubileeallianz_tz , sasa wakulima watapata bima ya mazao (Crop Insurance Cover) yenye kuwalinda dhidi ya hasara ya kuharibika kwa mazao itokanayo na madhara ya mabadiliko ya tabianchi kama vile hali mbaya ya hewa.
Mpango wa AfricaConnect uliozinduliwa mwaka 2022 chini ya Kampuni ya mbolea ya Yara ikiwa pamoja na benki ya @equitybanktz, Corteva Agriscience @Corteva, Wakala wa Taifa wa Uzalishaji Mbegu za kilimo @Agriculturalseedagency na kampuni ya Murzah Wilmar Rice Miller Ltd ambapo wakulima wa mpunga takriban 83,000 walinufaika kupata mafunzo na wakulima 4600 wa mikoa ya Kilimanjaro, Tanga, Morogoro, Arusha, Manyara na Iringa walinufaika kupata mbolea bora kutoka Yara, viwatilifu kutoka Corteva, huduma za ugani pamoja na huduma za kifedha ambapo benki ya Equity ilitoa mikopo yenye thamani ya shilingi 14 bilioni, na soko la mazao yao kupitia kampuni ya Murzah Wilmar Rice Miller Ltd.
Hata hivyo Mkurugenzi mkuu wa @Yaratanzania Bw. Winstone Odhiambo @agricpro ametangaza kutanua wigo na kuwezesha mpango huu kuweza kuwafikia wakulima zaidi ya 300,000 kwa mwaka 2023 na pia kuongeza mazao mengine ya mahindi, alizeti, viazi na kahawa kwenye mpango huu.
Tunawakaribisha wakulima kujiunga na mpango huu kupitia mawakala wa mbolea za Yara waliopo kote nchini, Mabwana/Bibi shamba wa Yara au kwa kutupigia namba yetu ya huduma kwa wateja 0800750188 Bure.
Негізгі бет Ғылым және технология Mpango wa AfricaConnect kuwawezesha wakulima wa Mpunga, Mahindi, Alizeti, Viazi na Kahawa sasa.
Пікірлер: 2