WAZIRI SILAA AZUI UTAPELI WA MABILIONI KARIAKOO
Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo na Makazi Mhe. Jerry Silaa amemuelekeza Kamishna wa Ardhi Msaidizi mkoa wa Dar es salaam na Msajili wa Hati Dar es salaam kuhakikisha wana mkabidhi hati yake ya umiliki wa ardhi mnunuzi wa awali wa nyumba aliyelipa Shilingi Bilioni 2.25 ili kuzuia kunyang'anywa na muuzaji ambaye amepata mnunuzi mwingine wa Bilioni 4.
Waziri Silaa ametoa maelekezo hayo ili kuzuia utapeli huo ambao alitaka kufanyiwa mnunuzi huyo wakati Waziri Silaa alipofanya ziara katika Kata ya Kariakoo mara baada ya kupokea malaamiko hayo.
Aidha, Waziri Silaa alingundua pia muuzaji huyo alileta shahidi wa uongo akidai ni mkewe wakati ni mtalaka wake.
Waziri Silaa pia amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara yake kuhakikisha yanafanyika marekebisho ya sheria za mikataba ya nyumba ya mwaka 2011.
Негізгі бет Ойын-сауық WAZIRI SILAA AZUIA UTAPELI WA MABILIONI KARIAKOO | ALIYELIPA BIL 2.25 ILI KUZUIA KUNYANG'ANYWA NA..
Пікірлер: 145