Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya makazi, Jerry Silaa amefanya ziara ya kushtukuza katika ofisi za kitengo cha Ardhi za halmashauri ya Jiji la Dodoma kwa ajili ya kujionea hali ya utendaji kazi ambapo amefika na kukuta baadhi ya watendaji hawajafika ofisini majira ya saa moja na nusu.
Waziri Jerry amewahimiza watumishi wa jiji la Dodoma na Tanzania kwa ujumla kuwa hasa watendaji wa ardhi kufika ofisini kwa muda uliopangwa na inapofika saa moja na nusu asubuhi huduma zianze kutolewa na si watu kuanza kuingia ofisini kwa wakati huo.
Негізгі бет WAZIRI JERRY SILAA ASHTUKIZA OFISI ZA ARDHI JIJINI DODOMA, ATOA MAELEKEZO KWA NCHI NZIMA
No video
Пікірлер: 203